Blogger Widgets
Esto music Tz | Members area : Register | Sign in

[NEWS]:RATIBA KAMILI YA MAZISHI YA ALBERT MANGWEA KUTOKA KWA KAKA WA MAREHEMU KENNETH

Friday, May 31, 2013

Share this history on :
Baada ya kumalizika kwa uchunguzi, uliokuwa ukifanyika
 katika hospitali ya Hillbrow, mwili wa marehemu Albert
 Mangwea(Pichani) unatarajiwa kuwasili Jumamosi kwa 
ndege ya Shirika la Ndege la Afrika ya kusini, 
ukitokea nchini Afrika ya kusini.
 Mwili utapelekwa moja kwa moja katika hospitali
 ya muhimbili kuhifadhiwa, uletwaji wa mwili huo, ni
 kwa hisani ya Clouds 
Media Group. Ndio waliogharimia safari ya 
mwili wa marehemu.

 Jumapili asubuhi, kuanzia saa mbili, mwili wa Albert
 Mangwea utakuwa unaagwa viwanja vya leaders 
club na kampuni 
itakayoshughulikia 
zoezi hili ni Entertainment Masters na baada
 ya mwili kuagwa, 
safari ya kumsindikiza Albert Mangwea 
kuelekea kwenye maziko
 itanza, na hii itakuwa ni kuelekea Morogoro.



Mwili wa Mangwea utazikwa Jumatatu katika eneo la
 Kihonda, mkoani,
Morogoro...!!
Ungana nasi Facebook Like page yetu hapa chini

Weka Maoni Yako Hapo Chini

Facebook Blogger Plugin by Esto Music Tz